HEBU TUVUNJE MBAVU KWA KUWA TUNA STRESS ZA MCHANA KUTWA

KUNA WIZI UMETOKEA BENKI
••••••••••••••• •••••••
Jambazi akasema "wote laleni chini pesa
ni za serikali na maisha ni ya kwenu",
wote wakalala chini (HII INAITWA
DHANA ...YA USHAWISHI - kubadilisha
njia ya
kawaida ya kufikiria)
••••••••••••••• •••••••
Kuna dada kwa woga akawa
amelala chini kimitego, Jambazi
akamwambia, "dada hebu kuwa
na adabu chukua kanga jifunike hili ni
tukio la ujambazi na sio la
ubakaji.” (HUU UNAITWA WELEDI -
zingatia ulichofundishwa kufanya)
••••••••••••••• ••••••••
Walipotoka kwenye
wizi jambazi mdogo ambaye ana shahada
ya uzamili ya biashara akamwambia
mwenzake, "tuzihesabu hizi fedha.” Yule
mkubwa akamcheka
kwa dharau na kumjibu, "wewe
mjinga sana hizo hazina haja ya
kuhesabu saa mbili wata tutangazia
kwenye taarifa ya habari tumeiba kiasi
gani. (HUU INAITWA UJUZI - Siku hizi
ujuzi ndio bora kuliko vyeti)
•••••••••••••••••••••••
Baada ya majambazi
kuondoka meneja akamwambia mhasibu
wa bank, " ujumlishie na zile milioni 80
tulizo iba sisi.” (HUKU KUNAITWA
KUOGELEA NA MKONDO WA MAJI -
kushabihiana na mazingira magumu kwa
faida binafsi.)
••••••••••••••• ••••••••
Mhasibu akafurahi na kusema, "dah wizi
ukitokea kila mwezi itakuwa burudani
sana.” (HUKU KUNAITWA KUWA NA
MAWAZO CHANYA - Furaha ndio kitu cha
muhimu zaidi)
••••••••••••••••••••••
Meneja kafurahi sana
kwa kuwa sasa matatizo yake
yametatuliwa
na wizi uliojitokeza. (HUKU KUNAITWA
KUTHUBUTU-shiki lia nafasi pale
inapojitokeza hata kama ni hatari kiasi
gani.
••••••••••••••• ••••••••
Haya usiku wake
taarifa ya habari
ikatangaza kuwa wizi mkubwa sana wa
million 100 umetokea leo benki.
Majambazi kuskia hivyo wakaanza
kuhesabu zile pesa lakini wakajikuta na
milioni 20 tu.
Yule jambazi mkubwa akashtuka na
kusema, "dah! yaani meneja kaiba mara
nne zaidi yetu bila kuchezesha msuli?
Bora umeneja kuliko ujambazi.” (HII
INAITWA
ELIMU NDIYO KILA KITU

Comments